WIZARA YAPOKEA MAGARI TISA KATI YA KUMI KURAHISISHA HUDUMA ZA KISHERIA KWA WANANCHI

 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akikata utepe kuashiria mapokezi na uzinduzi wa magari tisa kati ya kumi yatakayotumika katika kutoa huduma za Msaada wa Kisheria kwa Wananchi katika maeneo mbalimbali nchini. 20 Desemba, 2024.

Mwonekano wa magari tisa kati ya kumi yaliyopokelewa katika Wizara ya Katiba na Sheria kwa ajili ya kurahisisha utekelezaji wa shughuli za utoaji wa msaada wa kisheria kwa wananchi katika maeneo mbalimbali nchini. 20 Desemba, 2024.

Watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakiongozwa na Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro wakishangalia na kumkabidhi tuzo ya utendaji bora Katibu Mkuu wa Wizara Bw. Eliakim Maswi mara baada ya Wizara hiyo kushika nafasi ya pili katika Wizara zinazojali maslahi ya Watumishi. 20 Desemba, 2024.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damasi Ndumbaro amewataka watumishi wa wizara ya Katiba na Sheria kufanya kazi kwa weledi na ufanisi kutokana na Serikali kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya kurahisisha utendaji wao wa kazi.

Waziri Ndumbaro ameyasema hayo wakati akipokea magari tisa kwa ajili ya watumishi wa wizara hiyo katika kutekeleza Kampeni maalum ya Msaada wa kisheria ya Mama Samia Legal Aid campaign.

Amesema magari hayo yatasaidia kurahisisha utendaji kazi kwa Mikoa sita kwa wakati mmoja hivyo watendaji kuendelea kuwa waadilifu.

Magari tisa kati ya kumi yamezinduliwa tarehe 20 Desemba, 2024 ambapo lengo ni katika kurahisisha shughuli za utendaji kwa watumishi wa wizara hiyo.


Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA