WAZIRI NDUMBARO MGENI RASMI UZINDUZI WA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA MKOANI KIGOMA


 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji  Thobias Andengenye wakati Mhe. Waziri alipofika ofisini hapo kutoa salamu.

xxxxxxxxxxxxxxxxx

Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro leo tarehe 23 Januari, 2025 amewasili Mkoani Kigoma na kukutana na mwenyeji wake ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji  Thobias Andengenye, kwa ajili ya kushiriki katika Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia utakaofanyika tarehe 24 Januari, 2025 Mkoani Kigoma.

Akizungumza mara baada ya Mhe. Waziri kuwasili ofisini kwa Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya salamu, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma amesema kuwa ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kila Mwananchi anapata Haki na kwa wakati kupitia Kampeni ya Msaada wa Kisheria.

Kwa upande wake Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro amesema kuwa kupitia Kampeni ya Msaada wa Kisheria migogoro mbalimbali itakwenda kutatuliwa kupitia njia ya amani, usuluhishi, Mahakama, kiutawala na kwa njia za kiuchunguzi.

Mhe. Ndumbaro amesema kuwa, Kampeni ya Msaada wa Kisheria itatekelezwa kwa muda wa siku tisa katika Halmashauri tisa za Mkoa wa Kigoma na kuwafikia Wananchi katika maeneo mbalimbali ili kuhakikisha matatizo yote ya Kisheria yanapatiwa suluhu.

Comments

Popular posts from this blog

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA