KASI YA ELIMU YA KUANDIKA NA KUTUNZA WOSIA IONGEZWE

 


xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Katiba na Sheria kuongeza kasi katika kutoa elimu kuhusu umuhimu wa kuandika na kutunza wosia pamoja na kugawa mirathi kwa mujibu wa sheria ili kupunguza migogoro ya kijamii nchini.

Wakati akizindua kampeni ya Kitaifa ya msaada wa kisheria ya Mama Samia Mkoani Lindi, Waziri Mkuu pia amewaagiza wakuu wa wilaya kote nchini kuwatumia Mawakili wa serikali ngazi ya Wilaya, Halmashauri na Mikoa katika kuwa na programu mbalimbali za kusikiliza na kutatua kero za kisheria kwa wananchi ngazi ya Halamshauri.

Wakati wa hotuba yake Waziri Mkuu pia amewahimiza Viongozi wa dini na Viongozi wa kimila kuendelea kuhubiri na kuhimiza kuhusu upendo, Mshikamano na maadili mema kuanzia ngazi ya familia ili kuendelea kutunza amani, umoja na mshikamano wa jamii.

Waziri Mkuu Majaliwa ametumia fursa hiyo pia kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maamuzi yake ya kuanzisha na kugharamia kampeni ya msaada wa Kisheria ya Mama Samia ambayo kufikia mwezi Mei mwaka huu kampeni hiyo itakuwa imefanyika kwenye mikoa yote ya Tanzania bara na Tanzania Zanzibara ikiwa na lengo la kusaidia jamii dhidi ya changamoto mbalimbali za kisheria bila ya gharama.


Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA