MSLAC INATEKELEZA FALSAFA YA 4R ZA RAIS SAMIA

 


xxxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi ameitaja Kampeni ya kitaifa ya msaada wa Kisheria ya Mama Samia kuwa ya kipekee, mahususi na inayotekeleza sharti la kisheria la kuwa na msaada wa kisheria kwa wananchi na yenye kutekeleza kwa vitendo falsafa ya Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan ya 4R yenye kuhimiza kuhusu maridhiano na ujenzi wa Tanzania mpya.

Wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo mjini Ruangwa mkoani Lindi mbele ya Mgeni Rasmi Mhe. Kassim Majaliwa, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Prof. Kabudi amesema kwa Tanzania sharti la msaada wa kisheria limepanua wigo zaidi kwani linatoa msaada kwenye kesi zote ikiwemo zile za madai pamoja na jinai.

Prof. Kabudi ameitaja wizara ya Katiba na Sheria kuwa mtekelezaji mkubwa na msimamizi wa falsafa hiyo ya Rais Samia Suluhu Hassan, akimshukuru pia kwa kuasisi kampeni hiyo pamoja na uwezeshaji wake mkubwa alioutoa kuwezesha kampeni hiyo kuwafikia watu wengi zaidi hasa wale wa maeneo ya pembezoni na wasiokuwa na uwezo wa kiuchumi.

Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA