OFISI YA TAIFA YA MASHTAKA MWANZA YAHIMIZWA UWAJIBIKAJI


 xxxxxxxxxxxxxxxx

Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro Machi 18, 2025 Jijini Mwanza  ameongoza kikao na watumishi wa Ofisi ya Mwendesha Mashtaka wa  Mkoa huo ambapo amewahimiza umuhimu wa uwajibikaji katika kazi zao.

Akizungumza katika  kikao hicho, Mhe. Ndumbaro amesisitiza kwamba ni muhimu kwa watumishi hao kuongeza ufanisi ili kuboresha huduma wanazotoa kwa wananchi na  kusaidia katika utoaji wa Haki kwa wananchi.

Nae Mkuu wa Mashtaka wa Mkoa huo Bw. Joseph Mahugo, amemthibitishia Waziri Ndumbaro kwamba ofisi yake itaendelea kutoa huduma bora kwa maslahi ya taifa.

Ziara ya Waziri Ndumbaro Jijini Mwanza ina lengo la kufanya ukaguzi wa shughuli za ofisi hiyo na kuona jinsi wanavyoweza kuboresha huduma zao kwa umma.


Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA