SIMAMIENI MALALAMIKO YA UKIUKWAJI WA HAKI ZA BINADAMU - DKT. MWANDAMBO


 Watendaji wa Jiji la Tanga wakiwa katika picha ya pamoja na wawezeshaji kutoka Wizara ya Katiba na Sheria mara baada ya ufunguzi wa mafunzo ya Uraia na Utawala Bora yaliyofanyika tarehe 15 Machi, 2025.

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx

Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga Dkt. Stephen Mwandambo amewataka Watendaji wa Kata kusimamia malalamiko ya wananchi ya ukiukwaji wa Haki za Binadamu.

Dkt. Mwandambo ameyasema hayo tarehe 15 Machi, 2025 wakati akifungua mafunzo ya Uraia na Utawala Bora kwa Kamati ya Usalama Wilaya, Wakuu wa Idara na Vitengo pamoja  na Watendaji wa Kata wa Halmashauri ya Jiji la Tanga.

“Mafunzo haya yatamsaidia Mkurugenzi kutoa nafuu kwenye utekelezaji wa  majukumu na tunategemea kuona  huduma zimeboreshwa katika ngazi zote baada ya mafunzo haya.“

Mwandambo amesema kupitia mafunzo waliyopata watatekeleza kwa vitendo na kuhakikisha falsafa ya “4R“ ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inasambaa kutoka katika ngazi za chini mpaka za juu za uongozi.

Awali Wakili wa Serikali Kutoka Wizara ya katiba na Sheria na Mratibu wa Mafunzo Adv. Dorice Dario ameeleza malengo ya mafunzo hayo ni kuwawezesha Viongozi wa Serikali za Mitaa kuongeza ujuzi na maarifa yatakayo wasaidia kupokea na kushughulikia malalamiko ya wananchi yanayofikishwa mezani kwao.

Nao baadhi ya Watendaji wa Kata wameeleza kuwa mafunzo hayo yamekuwa na manufaa makubwa kwao, huku wakiahidi kuyatumia katika utekelezaji wa majukumu yao. Wakieleza kuwa uelewa mzuri wa sheria utawasaidia kusimamia haki na kuimarisha utulivu katika jamii.

Comments

Popular posts from this blog

USAJILI WA VIZAZI NA VIFO NI TAKWA LA KISHERIA

UONGOZI WA MAHAKAMA YA AFRIKA YA HAKI ZA BINADAMU NA WATU YAKUTANA NA VIONGOZI WA WIZARA YA KATIBA NA SHERIA

BODI YA KITAIFA YA USHAURI YA MSAADA WA KISHERIA YATEMBELEA WASAIDIZI WA KISHERIA IRINGA