Posts

Showing posts from September, 2020

MAZUNGUMZO YA AMANI YATAJWA KUWA NJIA BORA NA SALAMA YA UTATUZI WA MIGOGORO NCHINI.

Image
  XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Mazungumzo ya amani ni muarobaini uliothibitika kutumika kama tiba ya migogoro ya ardhi Mvomero Mkoani Morogoro.   Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Mvomero Mhe. Albinus Mgonya wakati akitoa taarifa ya hali ya amani wilayani humo kwa Kamati ya Kitaifa ya Ujenzi wa Amani na Kuzuia Mauaji ya Kimbari iliyofika walayani kwake hivi karibuni.   Wakulima na wafugaji ni watanzania wanaoishi pamoja na kushirikiana katika shughuli mbalimbali za kijamii, kisiasa na kiuchumi katika maeneo wanaoishi na zaidi, wengi wao ni wakulima na ni wafugaji kwa wakati mmoja hivyo njia ya mazungumzo ya amani imejipambanua kuwa tiba ya utatuzi wa migogoro inayowakabili.   "Unajua, hawa wakulima na wafugaji wanafahamiana kwasababu wanaishi pamoja, matumizi ya nguvu hususani vyombo vya ulinzi na usalama isingekuwa muarobaini, badala yake kwa kuwakutanisha na kuzungumza nao kumeonesha kuwa ni suluhisho la migogoro na ujenzi wa amani na utulivu baina yao.

PROF. MCHOME ATAKA WATANZANIA KUTUMIA VIZURI RASILIMALI ZILIZOPO NCHINI ILI KUJILETEA MAENDELEO

Image
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome akifungua kikao cha Makatibu Wakuu na Wakuu wa Taasisi cha kujadili Mfumo Jumuishi wa Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Rasilimali za Nchi kilichofanyika jijini Arusha. Washiriki wakichangia mada katika k ikao cha Makatibu Wakuu na Wakuu wa Taasisi cha kujadili Mfumo Jumuishi wa Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Rasilimali za Nchi.  Washiriki wakiendelea na kikao. Washiriki wa kikao wakiwa katika picha ya pamoja. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Nchi ya Tanzania imebarikiwa utajiri wa asili na rasilimali asilia ambazo zikitumika ipasavyo nchi na wananchi wake watakuwa na maendeleo ya kiuchumi. Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome wakati wa kikao cha Makatibu Wakuu na Wakuu wa Taasisi za Serikali waliokutana jijini Arusha kujadili Mfumo Jumuishi wa Uangalizi wa Utajiri wa Asili na Rasilimali za nchi. Profesa Mchome alisema Sheria ya Usimamizi wa Utajiri wa Asili na Maliasilia i

MAADILI KWA WATUMISHI WA UMMA NI TIBA YA AMANI NCHINI

Image
 XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Usimamizi thabiti wa maadili kwa watumishi wa umma katika kata na vijiji mkoani Morogoro umetajwa kuwa sababu ya kupunguza migogoro kati ya wakulima na wafugaji.   Hayo yamesemwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Morogoro Eng. Emmanuel N.M. Kalobelo alipotembelewa ofini kwake leo na Kamati ya Kitaifa ya Ujenzi wa Amani na Kuzuia Mauaji ya Kimbari.   Eng. Kalobelo amesema ukosefu wa maadili kwa watendaji wa kata na vijiji umeonekana kuwa kichocheo cha migogoro na uvunjifu wa amani katika maeneo mengi nchini lakini Serikali chini ya Mhe. Rais Dkt. John Joseph Pombe Magufuli imefanya kazi kubwa ya kulikomesha tatizo hilo mkoani Morogoro.   "Siku za nyuma Mkoa wa Morogoro ulikuwa kati ya mikoa yenye migogoro mingi ya ardhi kati ya wakulima na wafugaji lakini baada ya kufanya utafiti wa kina tukagundua watendaji na viongozi wa kata na vijiji walikuwa ndiyo chanzo kwani waliidhinisha uuzaji wa maeneo yasiyopimwa bila kufuata taratibu sahihi.

WATUMISHI WIZARA YA KATIBA NA SHERIA WASISITIZWA KULINDA MALI ZA UMMA

Image
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Prof. Sifuni Mchome ambaye ni mwenyekiti wa baraza la wafanyakazi la wizara hiyo akiongoza mkutano huo katika ukumbi wa mikutano wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro. Wajumbe wa baraza la wafanyakazi la Wizara ya Katiba na Sheria wakiendelea na mkutano huo. Zoezi la kuhesabu kura za uchaguzi wa Katibu wa baraza likiendelea. Katibu wa Baraza la wafanyakazi Wizara ya Katiba na Sheria Bi Basuta Milanzi (kushoto) akiwa na Katibu Msaidizi wa Baraza hilo Bw. Felix Chakila baada ya kuchaguliwa kushika nafasi hizo. Naibu Katibu Mkuu Ndg. Amon Mpanju akiwa amegusa kwa fimbo mchanga unaohama. Wajumbe wa Baraza la wafanyakazi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakiwa mbele ya mchanga unaohama. Nyumbu ni moja ya wanyama ambao ni vivutio vilivyopo katika bonde la Ngorongoro. XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wametakiwa kulinda mali za umma kama za kwao binafsi ili ziweze kudumu na kutumika kwa muda mrefu. Maelekezo hayo

KASI YA MAENDELEO YATAJWA KUWA KICHOCHEO CHA AMANI NCHINI

Image
  XXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXXX Kasi ya maendeleo yatajwa kuwa kichocheo cha amani nchini. Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Sumbawanga Dkt. Khalfan Haule alipotembelewa na Kamati ya Kitaifa ya Ujenzi wa Amani na Kuzuia Mauaji ya Kimbari ofisini kwake leo.   Dkt. Haule ametaja mafanikio yaliyofanywa na Rais wa Awamu ya Tano Mhe. Dkt. John Joseph Pombe Magufuli katika Sekta za Afya, Elimu, Barabara, Umeme, Maji na upatikanaji haki kwa wakati kuwa ni kichocheo cha ujenzi wa amani na utulivu hapa nchini.   "Huduma za jamii kama maji, elimu, umeme, afya, usafiri na usafirishaji ni haki ya msingi ya kila mwananchi. Naipongeza Serikali yangu chini ya Rais wetu mpendwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli kwa kuyapa kipaumbele masuala haya muhimu katika ujenzi wa amani na uchumi wa Taifa kwa kwa ujumla" amesema Dkt Haule.   Mwananchi akipata haki ya maendeleo kwa kuboreshewa na kusogezewa karibu huduma za jamii na nyingine hawezi kujihusisha na migogoro yo