Posts

Showing posts from January, 2025

WAZIRI NDUMBARO MGENI RASMI UZINDUZI WA KAMPENI YA MSAADA WA KISHERIA YA MAMA SAMIA MKOANI KIGOMA

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akisalimiana na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji   Thobias Andengenye wakati Mhe. Waziri alipofika ofisini hapo kutoa salamu. xxxxxxxxxxxxxxxxx Waziri wa Katiba na Sheria Dkt. Damas Ndumbaro leo tarehe 23 Januari, 2025 amewasili Mkoani Kigoma na kukutana na mwenyeji wake ambaye ni Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Kamishna Jenerali Mstaafu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji   Thobias Andengenye, kwa ajili ya kushiriki katika Uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia utakaofanyika tarehe 24 Januari, 2025 Mkoani Kigoma. Akizungumza mara baada ya Mhe. Waziri kuwasili ofisini kwa Mkuu wa Mkoa kwa ajili ya salamu, Mkuu wa Mkoa wa Kigoma amesema kuwa ameipongeza Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kazi kubwa anayoifanya ikiwa ni pamoja na kuhakikisha kila Mwananchi anapata Haki na kwa wakati kupiti...

WATOA HUDUMA ZA MSAADA WA KISHERIA 100 MKOANI MTWARA WAPIGWA MSASA

Image
  Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Bi. Bahati Geuzye akihutubia wakati akifungua kuanza kwa mafunzo ya Waratibu 100 wa Kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia (Samia Legal Aid campaign) kutoka Halmashauri tisa za mkoa wa Mtwara, tarehe 23 Januari, 2025. xxxxxxxxxxxxxxxx Waratibu 100 wa Kampeni ya msaada wa kisheria ya Mama Samia (Samia Legal Aid campaign) kutoka Halmashauri tisa za mkoa wa Mtwara wamepatiwa mafunzo ya utekelezaji wa kampeni hiyo   kuelekea kuanza kwa utoaji huduma ya kisheria kwa wakazi wa mkoa huo ambayo yataanza Januari 24 hadi Februari 2, mwaka huu. Akiongea wakati wa kuzindua mafunzo hayo Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara Bi. Bahati Geuzye amewataka waratibu hao kuhakikisha kwamba mafunzo wanayopatiwa kuhusiana na kampeni hiyo yanakuwa chachu na kuwawezesha kuwahudumia wananchi ambao kwa kiasi kikubwa wamekuwa na uhitaji wa kupata huduma za msaada wa kisheria ili kuwasaidia kutatua changamoto mbalimbali za kisheria zinazowakabili. Bi. Geuzye amesisiti...

MAZOEZI YA UTIMAMU WA MWILI KUELEKEA UZINDUZI WA MSLAC KATIKA MIKOA SITA.

Image
  Katibu Mkuu wa Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Eliakim Maswi katikati akiongoza mazoezi ya utimamu wa mwili kwa baadhi ya wajumbe wa Menejimenti na Watumishi wa Wizara hiyo Januari 16, 2025 Mtumba Jijini Dodoma ikiwa ni maandalizi ya kuelekea uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia katika Mikoa Sita. Baadhi ya Wajumbe wa Menejimenti na watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria wakiendelea na mazoezi ya viungo Januari 16, 2025 Mtumba Jijini Dodoma ikiwa ni maandalizi ya kuelekea uzinduzi wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria katia Mikoa sita.

WIZARA YAWAPIGA MSASA WARATIBU WA MSAADA WA KISHERIA NCHINI

Image
  Wizara ya Katiba na Sheria imetoa mafunzo kwa Waratibu wa Mikoa na Halmashauri kuhusu utekelezaji   wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia. Mafunzo hayo yameanza tarehe 14 Januari, 2025 katika Chuo cha Uongozi Mwl. Nyerere Kibaha, Pwani. Waratibu wa Mawakili wa Serikali, Wahadhiri Wasaidizi wa Vyuo Vikuu na Mawakili wa Kujitegemea kutoka Chama cha Mawakili Tanganyika (TLS) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya ufunguzi wa mafunzo kwa Waratibu wa Mikoa na Halmashauri kuhusu utekelezaji wa Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia. Mafunzo hayo yamefanyika kwa muda wa siku mbili katika Chuo cha Uongozi Mwl. Nyerere Kibaha, Pwani, tarehe 14 Januari, 2025. xxxxxxxxxxxxxxxxxx Wizara ya Katiba na Sheria imeendelea kuchukua hatua madhubuti katika kuhakikisha huduma za msaada wa kisheria kupitia Kampeni ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia (MSLAC) zinafikia Watanzania kwa ufanisi. Katika hatua ya kuimarisha utekelezaji wa kampeni hiyo, mafunzo maal...

VIJANA WATOA MSAADA WA KISHERIA WAMPONGEZA KM MASWI

Image
  Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria Bw. Eliakim Maswi akipokea zawadi kutoka kwa Vijana watoa Msaada wa Kisheria waliojiunga na Wizara ya Katiba na Sheria miezi minne iliyopita kwa ajili ya mafunzo kwa vitendo. Vijana hao wapatao 12 waliowakilishwa wameoneshwa kuguswa na utendaji kazi wa Katibu Mkuu na moyo wa kuwajali. T arehe 10 Januari, 2025 Mtumba, Dodoma. xxxxxxxxxxxxxxxxxxx Ikiwa ni miezi minne tangu vijana wapatao 12 wenye taaluma ya Sheria walipojiunga na Wizara ya Katiba na Sheria na kushirikiana na Wataalamu wa Wizara katika mafunzo kwa vitendo vijana hao wameonesha kuguswa na kumkabidhi zawadi ya pongezi Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Bw. Eliakim Maswi kwa utendaji kazi wake na moyo wa kuwajali. Wakizungumza mara baada ya kumtembelea Katibu Mkuu ofisini kwake Mtumba, jijini Dodoma leo tarehe 10 Januari, 2025 mwakilishi wa vijana hao  Prisila Kayuli amesema kuwa kwa kipindi chote wameshiriki na kupata ushirikiano ipasavyo katika shughuli mbalimbali za Wiza...

JAPAN KUSHIRIKIANA NA WIZARA KUENDELEZA SEKTA YA SHERIA NCHINI

Image
  Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akimkabidhi zawadi Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Yasushi Misawa wakati Balozi huyo alipomtembelea Waziri katika Ofisi za Wizara Mtumba, jijini Dodoma tarehe 8 Januari, 2025 kwa lengo la kumuaga baada ya kumaliza muda wake nchini. Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro akiwa ameambatana na ugeni kutoka Ubalozi wa Japan nchini Tanzania ukiongozwa na Mhe. Balozi Yasushi Misawa wakati alipomtembelea Waziri katika Ofisi za Wizara Mtumba jijini Dodoma tarehe 8 Januari, 2025 kwa lengo la kumuaga baada ya kumaliza muda wake nchini. xxxxxxxxxxxxxxxxxxx Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro leo tarehe 8 Januari, 2025 amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Japan nchini Tanzania Mhe. Yasushi Misawa alipomtembelea Mhe. Waziri katika Ofisi za Wizara Mtumba jijini Dodoma kwa lengo la kumuaga baada ya kumaliza muda wake nchini. Katika mazungumzo hayo yaliyohudhuriwa na Katibu Mkuu wa W...