KASI YA ELIMU YA KUANDIKA NA KUTUNZA WOSIA IONGEZWE

xxxxxxxxxxxxxxxxxxxx Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa ameiagiza Wizara ya Katiba na Sheria kuongeza kasi katika kutoa elimu kuhusu umuhimu wa kuandika na kutunza wosia pamoja na kugawa mirathi kwa mujibu wa sheria ili kupunguza migogoro ya kijamii nchini. Wakati akizindua kampeni ya Kitaifa ya msaada wa kisheria ya Mama Samia Mkoani Lindi, Waziri Mkuu pia amewaagiza wakuu wa wilaya kote nchini kuwatumia Mawakili wa serikali ngazi ya Wilaya, Halmashauri na Mikoa katika kuwa na programu mbalimbali za kusikiliza na kutatua kero za kisheria kwa wananchi ngazi ya Halamshauri. Wakati wa hotuba yake Waziri Mkuu pia amewahimiza Viongozi wa dini na Viongozi wa kimila kuendelea kuhubiri na kuhimiza kuhusu upendo, Mshikamano na maadili mema kuanzia ngazi ya familia ili kuendelea kutunza amani, umoja na mshikamano wa jamii. Waziri Mkuu Majaliwa ametumia fursa hiyo pia kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa maam...