4RS ZA RAIS SAMIA ZAITIKISA GENEVA

Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) ameongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano Tanzania kushiriki katika Kikao cha 58 cha Haki za Binadamu kinachofanyika Geneva Nchini Uswisi. 24 Februari, 2025. xxxxxxxxxxxxxxxxxx Akizungumza wakati akiiwakilisha Nchi ya Tanzania katika Kikao cha 58 Cha Haki za Binadamu kinachofanyika Geneva Nchini Uswisi tarehe 24 Februari, 2025 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Damas Ndumbaro (Mb) amesema kuwa, Nchi ya Tanzania imeendelea kuweka kipaumbele katika uendelezaji na ulinzi wa Haki za Binadamu katika utekelezaji wa shughuli za Serikali. Waziri Ndumbaro amesema kupitia Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,1977 na Katiba ya Zanzibar, 1984, Tanzania imeendelea kusimamia Utu wa Kibinadamu kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977 na Tamko la Kimataifa la Haki za Binadamu na inaendana na mkakati uliopitishwa na Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania M...